Thursday, July 28, 2016

Video: Genk anayochezea Samatta alivyoibuka ushindi Julai 28, 2016


KRC Genk wamekutana na Cork City, baada ya kuitoa Buducnost ya Montenegro kwa mikwaju ya penati 4-2, baada ya mechi yao ya mwisho kumalizika kwa Buducnost kuibuka na ushindi wa goli 2-0 ila kutokana na kuwa na aggregate ya 2-2 walilazimika kucheza dakika 120 na baadae mchezo ukaamuliwa kwa mikwaju ya penati.
licha ya KRC Genk kupata ushindi huo wakiwa pamoja na nyota wao kutokaTanzania Mbwana Samatta, bado wana wakati mgumu katika mchezo wa marudiano watakaocheza August 4 Ireland, kwani watakuwa wanahitaji ushindi au sare ya aina yoyote ile ili waweze kusonga mbele katika hatua inayofuata na kuitoa Cork City.

No comments:

Post a Comment