Sunday, July 31, 2016

Lowassa akutana uso kwa uso na Nape Nnauye kwenye msiba wa Mwandishi wa Tanzania Daima


Aliyekuwa mgombea urais kupitia Chadema na Ukawa, Edward Lowassa amekutana na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Mnauye leo katika jumuiko la kuuaga mwili wa aliyekuwa Mpigapicha wa Tanzania Daima, Joseph Senga. 

Mwili wa Joseph Senga (58) umesafirishwa leo kwenda nyumbani kwao, Shushi-Nyambichi, Kwimba mkoani Mwanza kwa ajili ya maziko hapo kesho.

Akizungumza wakati wa kuuga mwili wa marehemu Dar es Salaam mapema leo, msemaji wa familia, Charles Kapama amesema maziko yatafanyika kesho saa nane mchana baada ya mwili kuwasili kijijini.

Viongozi mbalimbali walijumuika na ndugu, jamaa na marafiki wa familia hiyo kuuga mwili wa marehemu Senga ambaye alifariki dunia Julai 27 katika hispitali ya BLK, New Dehli India alikokwenda kupatiwa matibabu, katika uwanja wa mpira uliojirani na nyumbani kwake, Sinza jijini hapa.

Viongozi hao ni pamoja na Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye, Mwenyekiti wa Chadema,  Freeman Mbowe, Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika na Mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea.
Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa Marehemu Joseph Senga, aliekuwa Mpiga Picha Mkuu wa Gazeti la Tanzania Daima, aliefariki Dunia hivi karibuni, wakati wa shughuli ya kuaga mwili huo, iliyofanyika katika Uwanja wa TP, Sinza Uzuri, Jijini Dar es salaam.
 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa Marehemu Joseph Senga, aliekuwa Mpiga Picha Mkuu wa Gazeti la Tanzania Daima, aliefariki Dunia hivi karibuni, wakati wa shughuli ya kuaga mwili huo, iliyofanyika katika Uwanja wa TP, Sinza Uzuri, Jijini Dar es salaam.
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa Marehemu Joseph Senga, aliekuwa Mpiga Picha Mkuu wa Gazeti la Tanzania Daima, aliefariki Dunia hivi karibuni, wakati wa shughuli ya kuaga mwili huo, iliyofanyika katika Uwanja wa TP, Sinza Uzuri, Jijini Dar es salaam.
 Jeneza lenye Mwili wa Marehemu Joseph Senga liwa katika Uwanja wa TP, Sinza Uzuri jijini Dar es salaam wakati wakiamuaga kwenda Kwimba, Mwanza kwa Maziko. Mwili wa Marehemu Joseph Senga unatarajiwa kuzikwa mara baada ya kufika.
 Familia ya Marehemu Joseph Senga ikiwa ni yenye huzuni kubwa kuondokewa na Mpendwa wao.
 Mbunge wa Jimbo la Ubungo, Said Kubenea akizungumza.
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe akizungumza.

Video: Goli la Samatta Ligi kuu Ubelgji July 31, 2016

Akitokea benchi zikiwa zimesalia dakika 10 mechi kumalizika, Mbwana Samatta amefunga bao lililoipa ushindi Genk kwenye mchezo wao wa kwanza wa ligi ya Ubelgiji (Belgium Pro League) na kuisaidia timu yake kupata ushindi wa magoli 2-1 wakati timu yake ikicheza dhidi ya KV Oostende.
Nikolaos Karelis alianza kufunga bao la kwanza dakika ya 50 kipindi cha pili kisha Mbwana Samatta akapachika bao la pili dakika ya 90+1.
Oostende walipata bao la kufutia machozi dakika ya 90+3 lililofungwa na Mzimbabwe Knowledge Musona na mpaka mwamuzi wa mechi hiyo anamaliza pambano hilo matokeo yakabaki Genk 2-1 Oostende.
Genk wamefanikiwa kupata pointi tatu na kukaa nafasi ya nne kwenye msimamo wa ligi baada ya kucheza mechi moja kwenye ligi hiyo ambayo ilianza msimu mpya jana Jumamosi. Timu ambazo zipo nafasi ya juu ya Genk zinatofautiana kwa tofauti ya magoli ya kufungwa na kufunga lakini pia herufi za kwanza za majina zimetumika kupanga ni timu gani ikae juu ya nyingine.

Kurasa za Magazeti: Leo Agosti 1, 2016 | Magazeti ya Tanzania

Pitia hapa kurasa za magazeti ya leo Agosti 1.
IMG_20160801_045451
IMG_20160801_045521
IMG_20160801_045536
IMG_20160801_045554
IMG_20160801_045609
IMG_20160801_045624
IMG_20160801_045640
IMG_20160801_045658
IMG_20160801_045728
IMG_20160801_045757
IMG_20160801_045814
IMG_20160801_045828
IMG_20160801_045844
IMG_20160801_045904
IMG_20160801_045917
IMG_20160801_045934
IMG_20160801_045955
IMG_20160801_050015
IMG_20160801_050040
IMG_20160801_050101
IMG_20160801_050116
IMG_20160801_050132
IMG_20160801_050148
IMG_20160801_050204
IMG_20160801_050225
IMG_20160801_050238
IMG_20160801_050258
IMG_20160801_050317

Friday, July 29, 2016

Kurasa za Magazeti: Leo Julai 30, 2016 | Magazeti ya Tanzania


Tarehe ya 30, Julai 2016 Jumamosi ya leo nakukariibisha kupitia kurasa za Magazeti ya Tanzania uweze kufahamu vichwa mbali mbali vya habari vinasema nini.

Karibu.....
IMG_20160730_050143
IMG_20160730_050205
IMG_20160730_050230
IMG_20160730_050253
IMG_20160730_050322
IMG_20160730_050345
IMG_20160730_050409
IMG_20160730_050437
IMG_20160730_050501
IMG_20160730_050527
IMG_20160730_050550
IMG_20160730_050615
IMG_20160730_050649
IMG_20160730_050712
IMG_20160730_050755
IMG_20160730_051555
IMG_20160730_051614
IMG_20160730_051638
IMG_20160730_051701
IMG_20160730_051727
IMG_20160730_051815
IMG_20160730_051847
IMG_20160730_051921
IMG_20160730_051937
IMG_20160730_052123