Friday, October 14, 2016

Aliyetobolewa macho aongezewa misaada zaidi

Nadhani unakumbuka vizuri ishu ya jamaa mmoja jijini Dar es Salaam Said Ally alivyoeleza namna alivyofanyiwa ukatili na kutobolewa macho yake mawili mbele ya umati wa watu katika eneo la Buguruni, watu wengi wamejitolea kwa hali na mali kumsaidia ili aweze kumudu gharama za maisha.
Said Ally ambaye alieleza stori yake kupitia kipindi cha Leo Tena cha Clouds Fm, watu wameweza kumchangia fedha, vitu vyakumsaidia kuendesha maisha yake na vitakavyomuingizia kipato kwa sababu hawezi tena kufanya kazi kutokana na kupoteza uwezo wa kuona baada ya kutobolewa macho.
Miongoni mwa misaada aliyoipokea hadi sasa ni pamoja na TZS milioni 10 ambazo amepewa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ambaye amesema kuwa yupo kwa ajili ya kuwasaidia wanyonge na wenye mahitaji kama alivyoagizwa na Rais Magufuli, lakini pia Makonda ameahidi kumlipia gharama aweze kufundishwa kusoma kwa kutumia alama na pia kumnunulia fimbo maalum ya kumsaidia kutembelea.
Mbali na Mkuu wa Mkoa, Said amepewa msaada wa pikipiki 5 ambapo kati ya hizo, pikipiki 2 ni msaada Infotech na pikipiki 3 ni msaada kutoka TSN. Pia Adamjee amemsaidia Said Bajaji mbili ambapo vyote hivi vitaweza kumsaidia kuingiza kipato na kuendesha maisha yake. Vitu vyote hivi vimepatikana kutokana na jitihada zilizofanywa na Mkuu wa Mkoa wa Dar wa kutafuta watu wa kumsaidia Said.
Kwa upande mwingine GSM kupitia ushawishi wa Mkuu wa Mkoa imesema kuwa itamsaidia Said Ally nyumba ya kuishi na yeye mwenyewe alishukuru sana  na kusema kuwa angependa nyumba hiyo iwepo maeneo ya Tabata, Dar es Salaam kwani ndilo eneo alilolizoea kwani amekua akiishi hapo tangu mwaka 1999.
Kwa upande mwingine, mwanamuziki Diamond Platnumz amejitolea msaada wa TZS milioni 2. Wakati Said akifanya mahojiano jana na Clouds Fm alisema kuwa moja ya vitu alivyo-miss kuvitazama ni pamoja na video ya Salome ya Diamond Platnumz, kitu kilichomsukuma mwanamuziki huyo kufika Clouds Fm na kutoa msaada.
Said Ally ambaye ni baba wa familia ya watoto 5, kabla ya kukumbwa na mkasa huo wa kuharibiwa macho yake na mtuhumiwa Scorpion alikuwa akifanya kazi ya kinyozi Tabata.
Mtuhumiwa aliyehusika na tukio hili tayari anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa uchunguzi kuweza kufanyika ili afikishwe mahakamani na haki iweze kupatikana.

Mwinyi asema ana wasiwasi na Tanzania tuliyopo

Ikiwa Tanzania leo inaadhimisha kumbukumbu ya miaka 17 tangu kufariki kwa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, Rais mstaafu wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi amesema ana wasiwasi na Taifa la sasa kwani halina uadilifu, aliotujengea Mwalimu Nyerere.Mwinyi aliyerithi mikoba ya urais kutoka kwa Mwalimu Nyerere mwaka 1985, alisema hayo jana jijini Dar es Salaam alipokuwa akifungua mdahalo wa kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere na kuzindua kitabu cha ‘Selective works of Mwalimu Nyerere’, kilichotafsiriwa na wasomi kutoka China.
Mdahalo huo uliandaliwa na Taasisi ya Uongozi ikishirikiana na Ubalozi wa China na Asasi ya Urafiki kati ya Tanzania na China. Mwalimu Nyerere aliyeitawala Tanzania kwa takribani miaka 24, alifariki dunia Oktoba 14, 1999 kwenye Hospitali ya St Thomas jijini London nchini Uingereza ambako alikuwa akitibiwa maradhi ya saratani ya damu.
Aliiongoza Tanzania kwa uadilifu mkubwa akisimamia misingi ya haki, umoja, mshikamano, kupiga vita rushwa, kusisitiza kujitegemea na uzalendo kwa nchi.
“Kazi za kawaida kweli zinafanywa na zinaendelea, lakini sina uhakika hata kidogo kama uadilifu aliotuachia Mwalimu bado tunao, sijui nani wa kulaumiwa,” alisema Mwinyi maarufu kama Mzee Ruksa. Alisema kwa namna ambavyo mambo yanakwenda, ni kiashiria tosha kuwa nchi haina uadilifu tena.
“Mambo yanavyokwenda kama gari lililo katika usukani,” alieleza Mwinyi na kuongeza kuwa kuna kila sababu ya kutafakari hali ilivyo sasa ikilinganishwa na ile ambayo iliachwa na Baba wa Taifa miaka hiyo 17 toka kufa kwake.
Alisema nafasi hiyo ya mazungumzo katika mdahalo, inawapasa kukaa kutafakari namna ya kurudisha nchi kwenye reli ambayo iliachwa na Mwalimu Nyerere ambaye ndiye muasisi wa taifa hili katika misingi ya uongozi.
“Tuna utajiri wa machoni, lakini ndiyo aliyokusudia Mwalimu? Alitufundisha tuwe matajiri wa vitu au matajiri wa moyo? Tujali vitu au tujali utu?” Alihoji Rais huyo mstaafu.

Isikupite hii ya diwani wa Chadema kunaswa na dawa za kulevya pamoja na bunduki


Jeshi la Polisi Mkoani Rukwa linamshikilia Diwani wa kata ya Izira, Paschael Silimba (Chadema) baada ya kumkamata akiwa na dawa za kulevya aina ya bangi na bunduki moja aina ya gobole.
Kamanda wa Polisi wa mkoa huo, Kamishna Msaidizi wa Polisi, George Kyando amesema kuwa jeshi hilo lilimkamata Kyando katika eneo la soko kuu ambalo hufanyia biashara yake ya kuuza mifuko ya salfeti, baada ya kupata taarifa na kuamua kumfuatilia.
Alisema kuwa baada ya kumpekua katika vifurushi vya bidhaa hiyo anayoiuza kwa kushirikiana na mkewe, walibaini uwepo wa bangi kiasi cha robo kilo.
“Baada ya kufanya upekuzi kwenye duka la diwani huyo, tumefanikiwa kukamata bangi kiasi cha robo kilo. Ni bangi kavu ambayo imeshaandaliwa tayari kwa ajili ya kufanya packing na kuuzwa,” alisema Kamanda Kyando.
Akizungumzia silaha aina ya gobole waliyoikuta nyumbani kwa diwani huyo anayodaiwa kuimiliki kinyume cha sheria, alisema ingawa ni silaha ya kizamani ina nguvu ya kuua tembo.
“Silaha hii ina nguvu sana, ina uwezo wa kuua tembo na ni hatari sana akipigwa binadamu kwa silaha hii. Kwahiyo msiione hapa mkaidharau, ina nguvu sana,” aliongeza.
Kamanda Kyando aliwataka viongozi wote waliopewa dhamana na wananchi kutotumia nyadhifa zao kufanya uhalifu. Alitoa wito wito kwa wananchi kuendelea kushirikiana na jeshi hilo kufichua uhalifu bila kujali waliofanya uhalifu huo.

Mbowe aahidi kuipeleka mahakamani serikali ya awamu ta tano

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, amesema atapeleka Serikaliya Awamu ya Tano mahakamani ili chombo hicho cha haki kitoe tafsiri ya vitendo vya ukandamizaji wa demokrasia vinavyofanywa na viongozi wa Serikali hasa Mkoani Arusha.
Mbowe ameyasema hayo alipokuwa akilaani kitendo cha Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, kuwasweka selo madiwani wanne wa chama hicho akisema kuwa hiyo ni ishara ya kwamba utawala wa awamu ya tano hauheshimu sheria.
“Nimewaagiza wanasheria wangu kwenda mahakamani ili kupata tafsiri sahihi kuhusu vitendo hivyo,” amesema.
Ameongeza kuwa viongozi hao wamekuwa wakifanya vitendo vya udhalilishaji kwa baadhi ya wabunge, madiwani, mameya na wenyeviti wa halmashauri kinyume na sheria.
“Nawashangaa sana Wakuu wa Mikoa na Wilaya wamekuwa wakiwadhalilisha wawakilishi wa wananchi ilhali wao wakiwa ni waajiriwa ambao hawajaomba kura kwa wananchi. Jambo hili limeanza mwaka huu, nah ii ni nafasi mbaya sana kwa Rais Magufuli kuchagua makada badala ya watumishi,” amefunguka Mbowe.

Kuhusu ishu ya makontena 100 kupitishwa Bandarini bila kukaguliwa, Waziri mwaijage katoa muda mchache wa wahusika kujisalimisha


Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Charles Mwijage ametoa siku nne kwa wafanyabiashara waliopitisha makontena 100 bandarini bila kukaguliwa na Shirika la Viwango Tanzania (TBS), wakatoe taarifa katika shirika.
Mwijage alitoa kauli hiyo jijini Dar es Salaam jana wakati akizungumza na waandishi wa habari baada ya kupata taarifa kuwepo kwa makontena 100, yaliyotolewa bandarini kwa siku zilizopita bila kukaguliwa na TBS.
“Nawataka wafanyabiashara wote waliochukua kontena hizo, wajisalimishe haraka TBS kabla ya kufika Jumanne ili wakaguliwe. Najua kuanzia kesho (leo) ni mapumziko, lakini TBS itaweka dawati la kuwasikiliza mpaka Jumatatu na ikifika Jumanne hatua zitachukuliwa kwa wahusika wote,” amesema Mwijage.
Alisema wafanyabiashara ambao hawatajisalimisha baada ya kumalizika kwa siku hizo, hatua stahiki zitachukuliwa ikiwemo kulipa faini ya asilimia 15.
Aidha, alisema kwa mawakala wa forodha wote, waliohusika kutoa kontena hizo wizara yake itawasiliana na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango ili kuona hatua za kuchukua kwa kuwa serikali haiwezi kukubali mchezo huo.
“Tayari tulishafunga michezo ya namna hii na tumeanza maisha mapya kwa hiyo mawakala na wote mliohusika kutoa kontena hizo sababu hazijafika mbali tunaomba mtueleze zilipo ili tukazikague,” aliongeza.
Pia alisema kontena hizo zilipaswa kukaguliwa na TBS, lakini baada ya tukio hilo kontena hizo zitakaguliwa na shirika hilo wakishirikiana na Tume ya Ushindani Tanzania (FCC).
 Aidha, amewaagiza TBS na FCC wafuatilie watu wao na kuziona bidhaa hizo, kwani watakaoshindwa hawatapewa cheti cha ubora bila kuona bidhaa na kukaguliwa.
“Sisi hatutaki mje mtueleze ni mzigo kiasi gani ili tupige penati hapana tunataka hilo kontena mlione na hiyo bidhaa muione na mkague,”aliongeza waziri huyo.
Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TBS, Dk Egid Mubofu alisema ni vyema wafanyabiashara hao wakafuata maagizo hayo na kujitokeza kukaguliwa ilikuepuka faini hiyo ya asilimia 15. 
Alisema upitishaji wa bidhaa bila kukaguliwa na shirika hilo unaweza kuleta madhara makubwa kwa watumiaji ambao hawajui kama bidhaa yako imekaguliwa ubora.
“Najua wafanyabiashara wengine watasema hatuendi kukaguliwa sababu hataitumia bidhaa hiyo, lakini anasahau kama anaweza siku moja na yeye akatumia bidhaa hiyo ambayo haijakaguliwa ni vyema wakawa wazalendo na kufuata maagizo waliyopewa,” alisema Mubofu.
TBS imeanzisha utaratibu mpya wa kulipisha faini mizigo inayoingia hapa nchini, ambayo haikukaguliwa wakati iko nchini China. Faini ni asilimia 15 ya thamani ya mzigo ulioingia.

Thursday, October 13, 2016

Kurasa za Magazeti: Leo Ijumaa Oktoba 14, 2016

Kuna habari mbali mbali zimeandikwa leo Ijumaa Oktoba 14, 2016 kwenye magazeti ya Tanzania na nje ya Tanzania. Hapa tuangalie kurasa za mbele na nyuma za magazeti ya leo Tanzania yameandika habari gani kisha tujadili pale chini kwa kuandika maoni yetu.

20161014_043132
20161014_043139
20161014_043146
20161014_043153
20161014_043159
20161014_043205
20161014_043211
20161014_043217
20161014_043224
20161014_043230
20161014_043257
20161014_043305
20161014_043312
20161014_043319
20161014_043324
20161014_043331
20161014_043337
20161014_043344
20161014_043358
20161014_043407
20161014_043413
20161014_043419
20161014_043425
20161014_043431
20161014_043437
20161014_043444
20161014_043450
20161014_043506
20161014_043513
20161014_043528
20161014_043535

Davido ft Tinashe - How Long | Listen and Download Mp3

Most anticipated video of the year off the SON OF MERCY EP from Davido is finally Out, This features international artist Tinashe .Watch!!



New Music Audio: Timaya ft Iyaz - How Many Times | Listen and Download Mp3

Timaya is here with a new Bang , this new record from the Egberi Papa just surfaced online.This new sound which is a leak is titled “How Many Times” and Iyaz is featured on this one with production credit from Kenny Wonder.


Wednesday, October 12, 2016

Kurasa za Magazeti: Leo Oktoba 13, 2016

Alhamisi ya Oktoba 13, 2016 kuna habari kem kem za kitaifa, kimataifa, biashara, udaku, burudani na michezo, kuna kurasa za magazeti mengi tu hapo chini kwa msaada wa Millardayo, karibu upitie kisha uache maoni yako.

20161013_043034
20161013_043041
20161013_043051
20161013_043059
20161013_043108
20161013_043115
20161013_043124
20161013_043132
20161013_043139
20161013_043145
20161013_043154
20161013_043200
20161013_043210
20161013_043216
20161013_043224
20161013_043230
20161013_043238
20161013_043246
20161013_043254
20161013_043303
20161013_043315
20161013_043321
20161013_043329
20161013_043336
20161013_043344
20161013_043349
20161013_043357
20161013_043404
20161013_043410
20161013_043416
20161013_043425
20161013_043433
20161013_043454
20161013_043501
20161013_043519