Friday, July 29, 2016

Tayari ratiba ya treni mpya Dar imetoka jijini Dar es Salaam


Uongozi wa kampuni ya reli Tanzania ‘TRL’ umetangaza kubadilishwa kwa muda wa kuondoka treni ya abiria kutoka Dar es salaam kwenda bara kuanzia August 02 2016, ambapo treni itaondoka saa 9 alasiri badala ya saa 11 jioni ilivyozoeleka.
Mabadiliko hayo yamefanyika ili kutoa nafasi kwa treni ya pili ya huduma ya jiji kutoka kituo kikuu cha reli cha Dar es salaam kwenda Pugu ambayo itaanza kutoa huduma Jumatatu Agosti Mosi, 2016.
Aidha huduma mpya ya treni ya jiji kwenda Pugu itakuwa na vituo 10 kama ifuatavyo,Pugu stesheni, mwisho walami, Gongo la mboto, FFU Mombasa, Banana njia panda kwenda Segerea) na Karakata, vingine ni pamoja na Vingunguti Mbuzi, SS Bakhressa, kamata na kituo kikuu cha reli Dar es salaam.
Huduma ya treni imeelezwa itakuwa ya awamu mbili asubuhi na alasiri ambapo treni ya kwanza itaondoka kituo cha Pugu saa 12 asubuhi na kuwasili kituo cha Dar es salaamsaa 12:55 asubuhi na kufanya safari 3 zitakazomalizika saa 05:15 asubuhi.
Jioni pia kutakuwa na safari 3 ambapo treni ya kwanza itaondoka kituo cha Dar es salaamsaa 09:55 alasiri kwenda pugu na kuwasili saa 10:50 jioni na safari ya mwisho kutoka Pugu kwenda Dar es salaam itakuwa saa 03:20 usiku.

No comments:

Post a Comment