Video ya wimbo huu unaokwenda kwa jina la Sidhani imeonyesha uelekeo mzuri mara baada ya waatazamaji kuongezeka kila baada ya dakika kadhaa, Siyo mbaya ukapata audio ya wimbo huu ambao umeimbwa na msanii Meda Classic akimshirikisha Timbulo.
Kati ya wasanii waliofanya vizuri kipindi fulani cha nyuma ni Matonya ambaye hapa katikati tunaona alikua kimya. Matonya amerudi na huu wimbo unaitwa Sugua Benchi, tuusikilize na tutoe maoni yetu.........
Tumezisikia nyimbo kadhaa kutoka kwa msanii Mwasity Almasi ikiwemo ile ya Unaniangalia, safari hii ameamua kumshirikisha binti machozi komando Jide na wanatuletea wimbo unaokwenda kwa jina la Wito.
Kupitia Redio na Tv msanii wa muziki wa kizazi kipya kwenye miondoko ya HipHop Kala Jeremiah aliahidi kutuletea wimbo mpya aliyomshirikisha mtoto ambaye tumezoea kumsikia kwenye nyimbo za dini Miriam Chirwa, Sasa ahadi ya Kala imekamilika na tayari wimbo huo hapo chini unaitwa Wana Ndoto.
Sikiliza na sema lolote kwa kuacha maoni yako pale chini...