Wednesday, February 1, 2017

Vanessa Mdee Kurudi Kibabe Mwezi Wa Nne

Mwanadada ambaye anatamba na kibao chake cha Cash Madamme, Vanessa Mdee amefunguka kwa kudai kuwa yeye ni mmoja kati ya wanawake ambao wanafanya kazi usiku na mchana ili kuhakikisha maisha yake yanaenda sawa.
Akiongea katika kipindi cha Wanawake Live cha EATV wiki hii, Vanessa amedai yeye ni mwanawake ambaye wanafanya kazi kwa bidii huku akidai tayari amejipangia ratiba ya kazi zake mpaka mwezi wa nne.
“Mimi nafanya kazi kama kichaa, kwa sababu kuna vitu ambavyo najua natakiwa nivitimize kwa muda fulani. Kwa hiyo najua nikivitimiza, nitakuwa na pesa ya kushoot video, pesa ya kuwekeza kwenye ardhi, na kupendeza kwa saababu kupendeza ni moja kati ya njia ya kuwekeza kwenye brand,” alisema Vanessa.
Aliongeza, “Lakini hayo yote hayaji bila kufanya kazi kwa bidii, kwa sababu mimi ratiba yangu kwa sasa ipo full mpaka mwezi wa nne, nimeshapanga kila kitu ambacho nitafanya kwa kipindi hichi,”
Muimbaji huyo kwa sasa anafanya vizuri na wimbo ‘Cash Madame’.

No comments:

Post a Comment